Tag: Adhabu

  • Ufafanuzi wa Aya Zenye Msamaha na Adhabu

    Ufafanuzi wa Aya Zenye Msamaha na Adhabu

    NIMEULIZWA NANUKUU:-

    Swali langu Al Habib Allah Katika quran katupa nafasi ya kuomba msamaha tunapokosea turejee kwake, na pia katuambia anasamehe madhambi yote, Aya nyengine anasema Allah hasamehi kushirikishwa lakini anasamehe yaliyo duni ya hayo kwa amtakaye Na aya nyengine anasema mwenye kumuua muumini kwa kukusudia malipo yake jahanam milele na laana ya Allah juu yake. Sasa suala langu msingi nataka kujua hizi aya ipi mansuh

    JIBU
    BISMILLAH

    Umeshapata MAJIBU katika Aya hizo zote. Hakuna zaidi.

    Acha nifafanue!

    1.Atayekufa bila ya kutubu hatia ya ushirikina HANA MSAMAHA.

    2.HAKI YOYOTE ILIYOPO BAINA YA MJA NA MOLA WAKE, INAWEZA KUSAMEHEWA NA MOLA WAKE, AKITUBU TOBA YA KWELI NA KURUDI KWA MOLA WAKE, KABLA YA KUFA KWAKE.

    3.HAKI YOYOTE ILIYOPO BAINA YA MWANADAMU NA MWANADAMU MWENZIWE, HAIWEZI KUSAMEHEWA ISIPOKUWA ALIYE DHULUMIWA ASAMEHE, VENGINEVYO ITALIPISHWA KWENYE MAHAKAMA YA MBINGUNI.

    4.HUKUMU YA KUMUUA MWISLAMU, PASI NA HAKI, NI KUUAWA ALIYEMUUA. AKIKIMBIA KUULIWA DUNIANI, AKAFA BILA YA KUTUBU, ATAISHIA KUINGIZWA MOTONI MILELE.

    FULL STOP.

    والله أعلم

    وبالله التوفيق