Nimeulizwa, NANUKUU:
“Habib Abdulqadir nina suala. Nini Hukumu ya kuvaa hirizi, au Kinga? Na Nini hukumu juu ya mwenye kutengeneza Hirizi hizo? Naomba ufafanuzi wa kina, maana ni tabia iliyozagaa sana katika jamii zetu.”
JIBU
BISMILLAH
Neno “Hirizi” lina maana pana, ila maana zote zinalenga katika kumaanisha KINGA, na hivyo hutumiwa kwa kitu chochote kile kinachoaminiwa kuwa ni kinga ya jambo baya, au jambo lisilotakiwa.
Kwa upande wa lugha, hirizi ni hifadhi au kinga ya jambo fulani. Neno jengine linalotumiwa ni حجاب hijab, طلاسم twalsam-twalasim,na عزيمة ‘aziima-‘aza’im yote yana maana moja ya kukinga, kulinda, kunusuru, kusitiri, kuchunga na kadhalika.
Na ni kutokana na maana hizo ndimo tunapata neno hijabu linalotumiwa kwa upande wa Sharia, kumaanisha vazi la kujisitiri, kwa Kiswahili ni Buibui, au kwa lugha ya siku hizi, ‘abaya. [ingawa hayo yanayoitwa ma’abaya yamegeuzwa, siku hizi, kuwa ni vivutio zaidi kuliko kuwa ni stara au hifadhi ya mwili والله المستعان ]
Kwa upande wa itikadi na imani, hata hivyo, tunapozungumzia Hirizi neno hilo linamaanisha kinga ya zindiko ili usifikwe na jambo fulani.
Iwapo zindiko hilo ni la maandishi maalum, basi maneno mengine yanayotumiwa –hata kwa Kiswahili- ni Talasimu, Azima, Hijabu, Zindiko na Sihiri.
Lakini, iwapo zindiko hilo linahusishwa na kitu maalum, kuwa kina nguvu za kukulinda na jambo fulani lisikufike, basi maneno yanayotumiwa, katika Kiswahili, ni Kago, Ndumba, Tunguri, Ndonga na Kinga. Ni maana hizo mbili: kinga ya maandishi na kinga ya kuamini kuwa kitu fulani chenyewe kina nguvu za kukulinda na jambo fulani au kukulinda na kitu fulani chengine, ndizo nitazozungumzia hapa.
A) Hirizi kwa maana ya kinga ya maandishi.
Kuna maadishi ya aina mbili, yanayo tumiwa katika kuandika hirizi.
a) Kwanza ni maandishi ya majina ya mashetani, majini au michoro ya mazingaombwe ya shaghala-baghala, wakidai kuwa ni kiatu cha Nabii Sulaiman, au Nyota ya kitu fulani, au sura za vitu maalumu, au nambari maalumu, ect., ect. Hizi ndizo zinazoitwa Talasimu, na Hirizi; kwa Kiarabu zinaitwa: تمائم au تولة. Hizi ni kufuru. Kiatu cha Nabii Sulaiman si kinga wala si dawa ya kitu chochote; iweje mchoro wake uwe kinga ya jambo lolote lile. Ubahalula. Uzandiki. Ujinga. Ulanguzi wa wadanganyifu wa kuwaibia na kuwala wajinga. Haramu kabisa, bali ni kufuru. Vile vile huitwa رقيا الشيطان au رقي tu.
b) Maandishi ya Qur’ani au Majina ya Mwenyezi Mungu na kadhalika. Haya huitwa حجاب الشرعي au الرقيا الشرعيHakuna junaha iwapo maandishi hayo ni Aya za Qur’ani au Majina ya Mwenyezi Mungu, kwa sharti kwamba pasiaminiwe kuwa MAANDISHI HAYO ndiyo yanayo kukinga au kukulinda. Bali mwenye kukukinga na kukulinda ni Mwenyezi Mungu aliyesema maneno hayo. Yaani unatumia Aya za Qur’ani au Majina Matakatifu ya Mwenyezi Mungu, kwa ajili ya kutabaruku tu, ukiamini kuwa mwenye kukinga na kulinda ni Mwenyezi Mungu,
Mwenyezi Mungu amesema, kuhusu Qur’ani:
﴿وَنُنَزِّلُ مِنَ الْقُرْآنِ مَا هُوَ شِفَاءٌ وَرَحْمَةٌ لِلْمُؤْمِنِينَ وَلا يَزِيدُ الظَّالِمِينَ إِلا خَسَارًا﴾ [الإسراء: 82].
Na tunateremsha katika Qur’ani yaliyo ni matibabu na rehema kwa Waumini. Wala hayawazidishii madhalimu ila khasara. (Al-Isra’, 17:82)
Na amesema, katika Surat Al-An‘am, Aya ya 155:
﴿وَهَذَا كِتَابٌ أَنْزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ فَاتَّبِعُوهُ وَاتَّقُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴾ [الأنعام: 155].
Na hiki ni Kitabu tulicho kiteremsha kilicho barikiwa. Basi kifuateni, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mrehemiwe. (Al-An‘am, 6:155)
عن محمد بن عبد الرحمن بن أبي ليلى عن عيسى أخيه قال: دخلت على عبد الله بن عكيم أبي معبد الجهني أعوده وبه حمرة فقلنا: ألا تعلق شيئًا؟ قال: الموت أقرب من ذلك، قال النبي صلى الله عليه وآله وسلم: «مَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا وُكِلَ إِلَيْهِ (رواه الترمذي وإبن ماجه )
Imepokewa kutoka kwa Abdurrhaman Ibn Abi Layla kutoka kwa Isa kutoka kwa ndugu yake akisema: “Nilimtembelea Abullah bin Ukaym; Abi Ma‘bad al-Juhaniyy, akiwa mgonjwa, akiwa amekaa na Hamza bin Abdil Muttalib (Ami yake Mtume ﷺ ). Tukamwambie kwanini huvai hirizi yoyote ile ya kujikinga? Akajibu kwa kusema: “Mauti yamesha nikaribia zaidi kuliko kufanya hivyo. Na nimemsikia Mtume ﷺ akisema: “Atayejifunga kitu (kama hirizi) ataachiwa nacho kimsaidie kama kinaweza kumsaidia.” Ameipokea Tirmidhi na Abu Daud.
Wanazuoni wameifasiri kuwa ukivaa kitu chochote kile, basi utaachiwa wewe na kitu chako hicho kikusaidie kama kinaweza kukusaidia; yaani utasokomezwa nacho. Hivyo, ukivaa maandishi ya Aya za Qur’ani basi Mwenyezi Mungu hatokusokomeza kwa asiyekuwa yeye akusaidie, bali atakusaidie yeye Mwenyewe, maana Qur’ani ni maneno Yake, ambayo ameyaelezea kuwa ni dawa na tiba na rehema.
Kwa maana hiyo, atayevaa au kujitundikia Aya za Qur’ani basi hawezi kuachiliwa na Mwenyezi Mungu asaidiwe na asiye kuwa Yeye; lazima atamsaidia Yeye mwenyewe kumtibu, kumlinda na kumhifadhi. Hivyo ndivyo walivyo fasiri wanazuoni wakubwa wakubwa wa Tafsiri za Qur’ani, kama Imam Al-Qurtuby katika Tafsiri yake: الجامع لأحكام الفرآن (10 :320 ) . Wengine ni Twabary, Ibn Kathiir na wengine.
عن عمرو بن شعيب عن أبيه عن جده: أن رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم قال: «إِذَا فَزِعَ أَحَدُكُمْ فِي النَّوْمِ فَلْيَقُلْ أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللهِ التَّامَّةِ مِنْ غَضَبِهِ وَعِقَابِهِ وَشَرِّ عِبَادِهِ وَمِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ وَأَنْ يَحْضُرُونِ؛ فَإِنَّهَا لَنْ تَضُرَّهُ». قال: وكان عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما يعلمها مَنْ بَلَغَ من ولده، ومَنْ لم يَبْلُغْ منهم كتبها في صك ثم علَّقَهَا في عُنُقِه رواه أبو داؤود والترمذي.
Vivyo hivyo, imepokewa kutoka kwa Amr bin Shu‘ayb kutoka kwa Baba yake kutoka kwa Bab u yake akisema: Amesema Mtume ﷺ : Akishtuka mmoja wenu usingizini kutokana na ndoto mbya, basi aseme: أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللهِ التَّامَّةِ مِنْ غَضَبِهِ وَعِقَابِهِ وَشَرِّ عِبَادِهِ وَمِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ وَأَنْ يَحْضُرُونِ؛ kwani hatosibiwa na kitu chochote, kile. Na amesema kuwa ‘Abdullah bin Amr رضي الله عنهما alikuwa akiwafundisha dua hiyo watoto wake waisome wanapo shtushwa na ndoto mbaya usingizini, na kwa wale ambao walikuwa bado hawakubalighi, basi alikuwa akiiandika dua hiyo kwenye karatasi na kuikunjakunja na kisha kuitundika shingoni mwa mtoto huyo.” Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi.
Hivyo, kitendo cha Sayyidina ‘Abdullah bin ‘Amr رضي الله عنهما kunukuu dua aliyofundisha Mtume ﷺ kujikinga na vitisho vya usingizini, na kuiandika kwenye karatasi na kisha kuitundika karatasi hiyo kwenye shingo ya watoto wake wadogo ni dalili kuwa inajuzu kuvaa hirizi ya dua ya kumuomba Mwenyezi Mungu, pekee, na kama dua inajuzu, basi Qur’ani inajuzu zaidi, maana Mwenyezi Mungu amesema kuwa Qur’ani ni dawa, uponesho na rehema kwa Waumini.
Vivyo hivyo, wafuasi wakubwa wakubwa wa Maswahaba wa Mtume ﷺ kama Ataa’, Mujahid na Sa‘id bin al-Musayyib رضي الله عنهم walikuwa wakiwaandikie watu hirizi za Aya za Qur’ani na dua za Mtume ﷺ na kuwapa wazivae kama hirizi. (Muswannaf In Abi shayba, juzuu ya 3, kurasa 43 hadi 44)
Imam Malik رحمه الله amesema: Hakuna junaha kuvaa hirizi za Aya za Qur’ani. Msimamo huo umeelezewa vile vile na wanazuoni wakubwa wakubwa, kama Ibn Hajar katika Fat-h al-Baary Sharh Swahih al-Bukhari, juzuu ya 6, ukurasa 142, alipokuwa akifafanua makatazo ya Hadithi yenye kukemea kuvaa hirizi za talasimu za maandishi yasiyokuwa Qur’ani ,kwa kusema:
هذا كله في تعليق التمائم وغيرها مما ليس فيه قرآن ونحوه، فأما ما فيه ذكر الله فلا نـهي فيه؛ فإنه إنـما يجعل للتبرك به والتعوذ بأسـمائه وذكره .
Makatazo yote haya ya hirizi za matalasimu ni kuhusu maandishi yasiyokuwa Qur’ani au yasiyokuwa majina ya Mwenyezi Mungu. Ama utajo (Qur’ani) wa Mwenyezi Mungu haukukatazwa; kwani Qur’ani imefafanuliwa na Mwenuezi Mungu kuwa inajuzu kutabaruku nayo na vile vile kujilinda kwa Majina Matakatifu ya Mwenyezi Mungu.
Na kuna Hadithi nyingi sana zinazosema kuwa inajuzu kujizingua kwa Aya za Qur’ani au dua maalumu za kuzingua, ambazo ametufundisha Mtume ﷺ . Na tofauti ya kuzingua na kujilinda, yaani hirizi ya maandishi ya Qur’ani ni kwamba kuzingua ni tiba baada ya kufikwa na tatizo; vile hirizi ni kinga usifikwe na matatizo; ila Aya ni zile zile, na maneno ni yale yale ya Mwenyezi Mungu. Hakuna junaha.
Kwa ufupi hakuna junaha kuandika au kuvaa hirizi za maandishi ya Aya za Qur’ani, au dua za Majina Matakatifu ya Mwenyezi Mungu, au hata dua zilizopokewa za kujilinda kutoka kwa Mtume ﷺ . Yaani dua ambazo hamna ushirikina wowote ndani yake, na hivyo kutabaruku na maneno ya Mwenyezi Mungu.
Ama maandishi yoyote mengine, yasiyokuwa hayo ni haramu,, kufuru na ushirikina. Na hayo ndiyo yale maandishi ya matalasimu ya majina ya mashetani, majini, picha za mazingaumbwe mbali mbali, michoro ya ramani, nyota, Mwezi, Jua,, na kadhalika, yote ni haramu, kufuru, haijuzu hata kidogo. Ni talasimu za kishetani na kufuru. Mwenyezi Mungu amesema:
وَاتَّبَعُوا مَا تَتْلُو الشَّيَاطِينُ عَلَىٰ مُلْكِ سُلَيْمَانَ ۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَانُ وَلَٰكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ وَمَا أُنزِلَ عَلَى الْمَلَكَيْنِ بِبَابِلَ هَارُوتَ وَمَارُوتَ ۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنْ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَا إِنَّمَا نَحْنُ فِتْنَةٌ فَلَا تَكْفُرْ ۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنْهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِ بَيْنَ الْمَرْءِ وَزَوْجِهِ ۚ وَمَا هُم بِضَارِّينَ بِهِ مِنْ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّهِ ۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ ۚ وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ وَلَبِئْسَ مَا شَرَوْا بِهِ أَنفُسَهُمْ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ (البقرة 2 :102)
_Nawakafuata yale waliyoyazua mashetani kuuzulia Ufalme wa Sulaiman. Na wala Sulaiman hakukufuru, bali mashetani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haatuta na Maaruta katika Baabil. Wala hao hawakumfundisha mtu yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru! Wakajifunza kutoka kwa hao wawili yale ya kumtenganisha mtu na mkewe. Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa utashi wa Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yanayo wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye chagua haya hatakuwa na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni uovu mno walio jiuzia nafsi zao; laiti wangelijua. (Al-Baqara, 2:102)_Na Mtume ﷺ amesema kuwa mazinguo ya talasimu za mashetani, na Shanga, Tunguri na kadhalika ni ushirikina.
إن الرقى والتمائم والتولة شرك “. رواه أحمد و أبو داود
“Mazinguo ya mashetani, Kago na Tunguri ni ushirikina.” Ameipokea Ahmad na Abu Daud.
B) Kinga nyengine, ambazo si za maandishi, ni kinga zinazoaminiwa kuhusiana na vitu mbali mbali, viwe venye roho au au visivyo na roho, kwa imani ya kuwa vitu hivyo, vyenyewe, vinakulinda na kukuhifadhi. Yaani itikadi potofu kuhusu vitu mbali mbali kuwa vina nguvuza kukulinda jambo fulani, au kukupatia manufaa fulani. Kinga za aina hii, kwa Kiarabu huitwa kwa majina mbali mbali, kama Tamaaim, Tiwala, Khazar, Wada’, na kadhalika, ambazo kwa Kiswahili ni sawa na maneno Kago, Ndumba, Tunguri, Ndonga, Zindiko, Fingo, Hijabu, Azima na kadhalika, Kinga za aina hii ni ushirikina na ukafiri uliokubuhu; maana ni kumtupilia mbali Mwenyezi Mungu kama alivyesema:
ثُمَّ إِذَا مَسَّكُمُ الضُّرُّ فَإِلَيْهِ تَجْأَرُونَ ثُمَّ إِذَا كَشَفَ الضُّرَّ عَنْكُمْ إِذَا فَرِيقٌ مِنْكُمْ بِرَبِّهِمْ يُشْرِكُونَ (النحل 16 : 54)
Na anapo kuondosheeni madhara, mara kundi moja miongoni mwenu, linamshirikisha Mola wao (An-Nahl, 16:54)
Na badala yake kugeukia kuamini kuwa Kago hizo zina nguvu ya kuwalinda, kukuhifadhi na kuwakinga na jambo lolote lile wasilo litaka liwafike, iwe kujikinga na maradhi, husuda, kijicho, shetani, jinni na kadhalika, au viwanufaishe na jambo lolote lile, kama kukupa utajiri, kwaharaka, biashara ichangamke, au kupasi mtihani na kadhalika. Ni ushirikina. Vyote hivyo ni Shirk. Haramu. Kufuru.
Mtume ﷺ amesema kuhusu Talasimu na Kago kwa aina zake zote:
((من تعلق تميمة فلا أتم الله له، ومن تعلق ودعة فلا ودع الله له، ومن تعلق تميمة فقد أشرك))[رواه أحمد وغيره )
Ataye vaa kinga basi Mwenyezi Mungu asimkinge. Na atayejivesha hirizi (tamiima) amemshirikisha Mwenyezi Mungu,” Ameipokea Ahmad na wengine.
عمران بن حصين “أن النبي صلى الله عليه وسلم أبصر على عضد رجل حلقة – قال: أراه قال: من صفر -، فقال: ويحك ما هذه قال من الواهنة قال: أما إنها لا تزيدك إلا وهنا، انبذها عنك، فإنك لو مت وهي عليك ما أفلحت أبدًا”2. ورواه ابن ماجة
Imepokewa kutoka kwa ‘Imraan bin Al-Huswayn رضي الله عنه akisema: Mtume ﷺ alimuona mtu amejifunga kikuku mkononi- nadhani cha shaba- akamuuliza: Ndiyo nini hiki? Akamibu kinaniondolea udhaifu. Mtume ﷺ akamwambia: Kwa kweli hakikuzidishii kitu ila udhaifu tu. Kivue ukitupilie mbali! Kwani lau kama utakufa na kikuku hicho kipo juu ya mwili wako basi hutaweza kuokoka hata kidogo.” Ameipokea Ibn Maja na Ahmad.
عن عقبة بن عامر الجهني “أن رسول اللّه صلى الله عليه وسلم أقبل إليه رهط فبايع تسعة وأمسك عن واحد. فقالوا: يا رسول اللّه، بايعت تسعة وأمسكت عن هذا؟ قال: إن عليه تميمة فأدخل يده فقطعها، فبايعه. وقال: من علق تميمة فقد أشرك”.( رواه أحمد والحاكم )
Imepokewa kutoka kwa ‘Uqba bin ‘Amir al-Juhaniyy رضي الله عنه akisema: Alikuwa Mtume ﷺ na kikundi cha watu 10. Basi akapokea Bay’a (Ahadi ya Utiifu) kutoka kwa watu tisa, lakini akajizuwia kumpa mkono mtu mmoja. Wale watu wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, umekubali Ahadi ya watu tisa, lakini umemkatalia huyu! Mtume ﷺ akasema: Kwa sababu amevaa Kago. Basi yule mtu akaingiza mkono wake na kuikata kamba ya ile Kago. Mtume ﷺ akampa mkono wa Bay’a, na kisha akasema: Anayejivesha Kago amemshirikisha Mwenyuezi Mungu.” Ameipokea Ahmad na Al-Hakim.
Naam, hakuna junaha ikiwa una maradhi maalumu, kama upungufu wa madini fulani,, mwilini, na madaktari wakakuambia kuwa unahitaji kuongeza madini fulani mwilini mwako, na wakapendekeza kutumia dawa maalumu, au kuvaa kitu maalumu kitacho kusaidia kupata hayo madini unayohitajia, basi hakuna junaha. Maana hapo una matatizo ya upungufu wa kitu fulani mwilini mwako na madaktari wamekupa njia ya kujitibu. Huko si kuamini kuwa hicho ulichovaa ndicho kinacho kusaidia, bali ni kuamini kuwa umepewa dawa ya matatizo yako ya kiafya. Ni sawa na kuandikiwa virutubisho fulani mwilini, kama Vitamin C. Hakuna junaha hapo.
Kuna hadithi nyingi za kuharamisha kutumia vitu vyovyote vile kwa imani kuwa vitu hivyo vyenyewe, ndio kinga, au hirizi inayo kulinda na kukuhifadhi, au hata kukunufaisha kitu fulani. Miongoni mwa kago hizo, za kishirikina, katika nchi zetu za Afrika ya Mashariki na kwengineko, ni Makucha ya Simba, Kaure za pwani, Shanga, Mafupa ya wafu, Mafuvu ya maiti, nywele za mkia wa simba au tembo, meno ya papa, au ya simba, kucha za kima, meno ya sokwe, mafupa ya albino, ngozi ya albino, damu ya hedhi (wanaita Limbwata), pembe za wanyama mbali mbali na kadhalika. Vyote hivyo vinaingia katika jina la Kago, Ndunguri, Hijabu, Pagao, Hirizi, Zindiko, Sihiri, Kinga, Fingo, Lindo na kadhalika na vyote ni harmu, ushirikina na kufuru. Mwenye kuvaa ili vimlinde amekufuru. Mwenye kuvitengeneza na kuwapa watu wavivae ili viwalinde amekufuru maradufu.
والله أعلم
وبالله التوفيق
السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
Imejbiwa na Sayyid Abdulqadir Shareef
NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chchote, na kuweka kwenye FB yako au kwenye WhatsApp na kwenye Makundi ya Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, kwa lengo la kusambaza na kuelimisha Dini. Changia kusambaza Dini, ujipatie thawabu.
kcwajawema@gmail.com
Leave a Reply