(10)
كِتَاب أبْوَابِ الأَذَانِ
KITABU CHA MILANGO YA ADHANA
31- بَاب: مَنْ صَلَّى بِالنَّاسِ وَهُوَ لَا يُرِيدُ إِلَّا أَنْ يُعَلِّمَهُمْ صَلَاةَ النَّبِيِّ ﷺ وَسُنَّتَهُ
- Mlango: Kuhusu mtu anayewaswalisha watu na lengo lake lilikuwa ni kutaka kuwafundisha tu swala ya mtume ﷺ na sunna zake
405- عَنْ مَالِكُ بْنُ الْحُوَيْرِثِ رضي الله عنه قَالَ: إِنِّي لأصَلِّي بِكُمْ وَمَا أُرِيدُ الصَّلاَةَ، أُصَلِّي كَيْفَ رَأَيْتُ النَّبِيَّ ﷺ يُصَلِّي. [رواه البخاري: 677].
- Imepokewa kutoka kwa Malik bin Huwayrith رضي الله عنه akisema: “Mimi ninakuswalisheni na lengo langu siyo mimi kuswali lakini nakuswalisheni nikuonyesheni vipi nimemuona Mtume ﷺ anaswali.” [Bukhari: 677]
32- بَاب: أَهْلُ الْعِلْمِ وَالْفَضْلِ أَحَقُّ بِالْإِمَامَةِ
- Mlango: Wanawazuoni na wenye fadhila wanastahiki zaidi kuongoza swala
406- عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهَا حَدِيثُ: «مُرُوا أَبَا بَكْرٍ يُصَلِّي بِالنَّاسِ»تَقَدَّمَ،( ) وَفِي هذِهِ الرِّوايَةِ قَالَتْ: قُلْتُ: إِنَّ أَبَا بَكْرٍ إِذَا قَامَ فِي مَقَامِكَ، لَمْ يُسْمِعْ النَّاسَ مِنْ الْبُكَاءِ، فَمُرْ عُمَرَ فَلْيُصَلِّ لِلنَّاسِ. فَقَالَتْ عَائِشَةُ: فَقُلْتُ لِحَفْصَةَ: قُولِي لَهُ: إِنَّ أَبَا بَكْرٍ إِذَا قَامَ فِي مَقَامِكَ، لَمْ يُسْمِعْ النَّاسَ مِنْ الْبُكَاءِ، فَمُرْ عُمَرَ فَلْيُصَلِّ لِلنَّاسِ، فَفَعَلَتْ حَفْصَةُ، فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ: «مَهْ، إِنَّكُنَّ لاَنْتُنَّ صَوَاحِبُ يُوسُفَ، مُرُوا أَبَا بَكْرٍ فَلْيُصَلِّ لِلنَّاسِ» فَقَالَتْ حَفْصَةُ لِعَائِشَةَ: مَا كُنْتُ لِأُصِيبَ مِنْكِ خَيْرًا. [رواه البخاري: 679].
- Imepokewa kutoka kwa Aisha رضي الله عنها na hii ni hadithi ndefu ambayo Mtume ﷺ anaripotiwa kusema: “Muamrisheni Abu Bakr akawaswalishe watu” imeshatangulia. Katika riwaya hii ya hapa anasema Aisha رضي الله عنها : “Nikamwambia Mtume ﷺ : Kama Abu Bakr atakuqaimu kuswalisha basi watu hawatomsikia kitu kutokana na kulia kwake bora umuamrishe Umar awaswalishe watu” anasema Aishaرضي الله عنها : Nikamnong’oneza Hafswa رضي الله عنها amwambie mtume ﷺ maneno hayo hayo kwamba Abu Bakr akikuqaimu katika swala watu hawataweza kumsikia kitu kutokana na kulia kwake kwa hivyo Muamrishe Umar awaswalishe watu, Hafswa akafanya akaenda kumwambia mtume ﷺ , Mtume ﷺ alipoambiwa maneno hayo ambayo keshayasikia kutoka kwa Aisha alimuambia Hafswa: “Nyamaza! Acha nyinyi mmekuwa kama wanawake wa Nabii Yusuf, nimesema muamrisheni Abu Bakr awaswalishe watu” anasema Hafswa: akamrudia Aisha na kumwambia: “Sijapata jambo lolote kutoka kwako wewe lenye khayr.” [Bukhari: 679]
407- عَنْ أَنَسُ رضي الله عنه : أَنَّ أَبَا بَكْرٍ كَانَ يُصَلِّي لَهُمْ فِي وَجَعِ النَّبِيِّ ﷺ الَّذِي تُوُفِّيَ فِيهِ، حَتَّى إِذَا كَانَ يَوْمُ الِإثْنَيْنِ، وَهُمْ صُفُوفٌ فِي الصَّلاَةِ، فَكَشَفَ النَّبِيُّ ﷺ سِتْرَ الْحُجْرَةِ، يَنْظُرُ إِلَيْنَا وَهُوَ قَائِمٌ، كَأَنَّ وَجْهَهُ وَرَقَةُ مُصْحَفٍ، ثُمَّ تَبَسَّمَ يَضْحَكُ، فَهَمَمْنَا أَنْ نَفْتَتِنَ مِنْ الْفَرَحِ بِرُؤْيَةِ النَّبِيِّ ﷺ ، فَنَكَصَ أَبُو بَكْرٍ عَلَى عَقِبَيْهِ لِيَصِلَ الصَّفَّ، وَظَنَّ أَنَّ النَّبِيَّ ﷺ خَارِجٌ إِلَى الصَّلاَةِ، فَأَشَارَ إِلَيْنَا النَّبِيُّ ﷺ أَنْ أَتِمُّوا صَلاَتَكُمْ وَأَرْخَى السِّتْرَ، فَتُوُفِّيَ مِنْ يَوْمِهِ. [رواه البخاري: 680].
- Imepokewa kutoka kwa Anas رضي الله عنه akisema: “Pale Abu Bakr alipokuwa anawaswalisha watu kutokana na maradhi aliyokuwa nayo mtume ﷺ ambayo ndiyo yaliyompelekea mpaka akafariki, ilipofika siku ya Jumatatu na watu wamejipanga swafu msikitini wanaswali Mtume ﷺ alifunhua pazia kutoka chumbani kwake akaangalia msikitini akatuangalia msikiti na yeye amesimama chumbani kwake, uso wake una ng’ara utafikiri karatasi ya Mus’haf kisha akatabasamu na kucheka, tukataka kufitinika kutoka na furaha ya kumuona mtume ﷺ , Abu Bakr akarudi kinyume nyuma ili akajiunge na swafu alidhani kwamba mtume ﷺ atatoka kuja kuswalisha lakini mtume ﷺ akaashiria kwa mkono wake kwetu sisi kwamba timizeni swala kisha akalifunga pazia lake na siku hiyo ndiyo aliyofariki.” [Bukhari: 680]
KUTOKA *UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY *
*HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO! *
*JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO! *
TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu!
من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
خادم السنة النبوية
Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
*MTumishi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, na kuweka kwenye FB yako, WhatsApp, na kwenye Makundi ya Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, kwa lengo la kusambaza na kuelimisha Dini. Changia kusambaza Dini, ujipatie thawabu.
kcwajawema@gmail.com