Hadithi ya Leo, Jumatano, tarehe 13, Shaabani, 1446, sawa na tarehe 12, JANUARI, 2025
KUHUSU KUCHINJA MNYAMA WA AQIQA
SEHEMU YA KUMI NA PILI
1357 – وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا { أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَمْرَهُمْ أَنْ يُعَقَّ عَنْ اَلْغُلَامِ شَاتَانِ مُكَافِئَتَانِ، وَعَنْ اَلْجَارِيَةِ شَاةٌ } رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَه .
- Imepokewa kutoka kwa ‘Aisha رضي الله عنها akisema: “Mtume aliwaamrisha watu wachinje mbuzi wawili wa aina moja, wenye kufanana kwa ajili ya mvulana na mbuzi mmoja kwa msichana.” Ameisahihisha Tirmidhi na kusema ni Hadithi Sahihi.
1358 – *وَأَخْرَجَ اَلْخَمْسَة ُ عَنْ أُمِّ كُرْزٍ الْكَعْبِيَّةِ نَحْوَه *ُ. - Imepokewa kutoka kwa Ummu Kursi رضي الله عنها sawa na hadithi ya hapo juu.
UFAFANUZI
Hadithi hii kutoka kwa Mama Aisha رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا inasema kuwa Mtume ﷺ aliwaamrisha Maswahaba wake wawachinjie watoto wao wa kiume mbazi wawili wawili, kila mmoja, na mbuzi hao wawe wanafanana kwa kila kitu, umri, uzima na kadhalika. Na wawachinjie watoto wao wa kike mbuzi mmoja, kila mmoja. Hivyo, Hadithi hii inatuondolea mushkeli wa idadi ya wanyama wa Aqiqa wanaotakikana kuchinjiwa watoto na wazee wao, ama iwe kwa kiwango cha chini, ambapo kila mtoto achinjiwe mbuzi au kondoo mmoja mmoja, au kiwango cha juu, ambapo kila mtoto wa kiume achinjiwe mbuzi au kondoo wawili, vile mtoto wa kike anatakiwa achinjiwe kondoo au mbuzi mmoja.
Wanazuoni, wakazidi kutufafanulia kwa kusema:
الحكمة في تمييز الذكر عن الأنثى أنَّ العقيقة هي نسيكة شكر لله تعالى على نعمة تجدد المولود، ولما كان الذكر أعظم نعمة، وامتنانًا من الله تعالى، كان الشكر عليه أكثر، فصار له شاتان، وللجارية شاة
Na hekima ya kuwepo tofauti baina ya mtoto wa kiume na mtoto wa kike, katika kuwachinjia wanyama wa Aqiqa, ni kuwa Aqiqa ni Ibada ya نسيكة UCHAMUNGU wa utaratibu maalumu na wakati maalumu, katika kumshukuru Mwenyezi Mugu kwa neema ya kupewa mtoto wa kiume, ambaye ndiye atakuja kuwa mwenye kuendeleza kizazi cha Baba mchinjaji na kutunza nasaba yake kwa siku za usoni, na hivyo hiyo ni neema kubwa sana kupewa Baba mtu na Mola wake, na kila neema ikizidi ukubwa wake, basi na shukrani zake nazo zinakuwa kubwa zaidi. Ndiyo maana, mtoto wa kiume anatakiwa achinjiwe mbuzi au kondoo wawili, vile mtoto wa kike, ambaye bado ni neema vile vile, ila yeye hatokuwa muendelezaji wa ukoo wa Baba yake, bali atakuwa muendelezaji wa ukoo wa mumewe, ndiyo maana shukrani zake ni kuchinjia na Baba yake kondoo au mbuzi mmoja. Hakuna, junaha, hata hivyo, kuchinjiwa mtoto wa kike kondoo au mbuzi wawili vile vile. Kwa maneno mengine, uchinjaji wa Aqiqa kwa ajili ya mtoto wa kiume, ni نسك Ibada ya Uchamungu, yenye utaratibu wake maalumu, kama zilivyo Ibada za Hija na Umra, vile uchinjaji wa Aqiqa kwa mtoto wa kike ni Sadaka; haina utaratibu maalumu wala wakati maalumu
YALIYOMO NA YATOKANAYO
- Hadithi hii ni dalili nyengine kuwa Asasi ya Aqiqa ni Asasi halali iiyothibiti kupitia amri ya Mtume ﷺ kwa wafuasi wa Umma wake.
- Mtume ﷺ ameamrisha mtoto wa kiume achinjiwe mbuzi au kondoo wawili, na mtoto wa kike achinjiwe mbuzi au kondoo mmoja.
- Hadithi ni dalili, vile vile, kuwa Si kila amri inamaanisha wajibu kuitekeleza, maana hakujatajwa adhabu au dhambi yoyote kwa asiyechinja.
- Zaidi, ni kuwa kuna Riwaya nyingi zenye kuonesha kuwa kuchinja mnyama wa Aqiqa ni Sunna iliyotiiwa mkazo, si lazima kuchinja.
- Kuna tofauti baina ya نسك na صدقة. Nusuk ni Ibada ya vitendo inayotakiwa kutekelezwa kwa wakati wake kama alivyo itetekeleza Mtume ﷺ Vile Sadaka ni ibada ya vitendo, vile vile, ila haina wakati wake maalumu, wala utaratibu maalum, na ni Ibada ya kujitolea.
- Kuchinja wanyama wa Aqiqa kwa mtoto wa kiume ni Nusuk , lakini kuchinja mnyama wa Aqiqa kwa mtoto wa kike ni Sadaka.
- Si Sunna kumnyoa nywele mtoto wa kike; Mtume ﷺ hakuwanyoa wajukuu zake wa kike, kama Umama binti Abi-Al’as bin Ar-Rabi’, mjukuu wa Zainab binti Muhammad, mtoto mkubwa wa Mtume ﷺ.
- Baadhi ya wanazuoni, hata hivyo, wamechukua msimamo wa kumnyoa nywele mtoto wa kike, vile vile, baada ya kumchinjia mnyama wa Aqiqa.
والله أعلم
وبالله التوفيق
HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO
IMETAYARISHWA na Sayyid Abdulqadir Shareef
*Mtumishi wa Sunna za Mtume ﷺ *
من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
خادم السنة النبوية
KUTOKA KITABU CHA بلوغ المرام من أدلة الأحكام UFIKIAJI WA MALENGO KUPITIA HADITHI ZA FIQHI YA MILANGO
JIUNGE NA KUMBI ZA DARSA ZA SAYYID ABDULQADIR SHAREEF, KWA KUTUMA MAOMBI YAKO, MOJA KWA MOJA, KWENDA NAMBA +255786887887, KUPITIA WHATSAP
LAZIMA UTAJE MAJINA YAKO HALISI MATATU NA MAHALI ULIPO! SHARIA ZA MITANDAO TANZANIA
UKIWA NA SUALA LOLOTE, LINALOKUHUSU WEWE MWENYEWE, NA SI KUMHUSU MTU MWENGINE, USIMTUMIE MWENYE KUTOA DARSA, BALI MTUMIE ADMIN WA UKUMBI WAKO, AKUPATIE JIBU, KAMA LIPO JIBU LAKE, KUTOKANA NA MAJIBU ZAIDI YA 3000, AU ALIWEKE SUALA LAKO KUMBINI, LISUBIRI KUJIBIWA USIMTUMIEA MTOA DARSA
NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, na kuweka kwenye FB yako, WhatsApp, na kwenye Makundi ya Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, kwa lengo la kusambaza na kuelimisha Dini. Changia kusambaza Dini, ujipatie thawabu.
kcwajawema@gmail.com