Category: Hadith

  • NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME ﷺLeo Jumaane, tarehe 19 SHAABANI, 1446, H., sawa na tarehe 18, FEBRUARI, 2025WASIA WA 58مئتا وصية من وصايا الرسول ﷺجمعها ورتبها ثم فسرها إلى السواحليةالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME *ﷺ.Zimekusanywa na Kufasiriwa kwa Kiswahili naSayyid Abdulqadir ShareefMTIMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    الوصية الثامنة والخمسون
    لا يَقُولَنَّ أَحَدُكُمْ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي إِنْ شِئْتَ
    58: “Kamwe, asiombe mmoja wenu kwa kusema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nifutie dhambi zangu Ukipenda

    *عنْ أَبي هُريْرَةَ رَضِيَ اللَّه عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ ﷺ قَالَ : « لا يَقُولَنَّ أَحَدُكُمْ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي إِنْ شِئْتَ : اللَّهُمَّ ارْحَمْني إِنْ شِئْتَ ، لِيعْزِمِ المَسْأَلَةَ ، فإِنَّهُ لا مُكْرِهَ لَهُ » متفـــقٌ عليه. وفي روايةٍ لمُسْلِمٍ : « وَلكنْ ، لِيَعْزِمْ وَلْيُعْظِّمِ الرَّغْبَةَ ، فَإِنَّ اللَّه تَعَالى لا يتَعَاظَمُهُ شَـيْءٌ أَعْطَاهُ » *

     Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra *رضي الله عنه* akisema: “Amesema Mtume ﷺ: “Kamwe, asiombe mmoja wenu kwa kusema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nifutie dhambi zangu Ukipenda! Nifutie dhambi zangu Ukipenda! Bali aombe kwa dhati na kukuza maombi yake; kwani hakuna wa kumteza nguvu Mwenyezi Mungu!” _Muttafaq ‘alayhi_ Yaani mtu akiomba aombe kwa dhati na kwa nia safi kabisa, na asijaribu kushinikiza tu. 

    KUTOKA NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIYA YA MTUME ﷺ
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu
    kcwajawema@gmail.com

  • TAFSIRI YA UFUPISHO WA KITABU CHA SWAHIHIL-BUKHARIمختصر صحيح البخاري للزبيديرتبه ثم فسره إلى السواحلية ووضع بعض تعليقاتالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*TAFSIRI YA UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY.*Kimetayarishwa kisha Kufasiriwa kwa Kiswahili *Sayyid Abdulqadir ShareefMTUMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    Leo Siku ya Jumatatu, tarehe 18, Shaaban 1446, H., sawa na tarehe 17 Februari, 2025.

    23- بَاب: مِنْ أَيْنَ يَخْرُجُ مِنْ مَكَّةَ

    1. Mlango: Je mtu anapoondoka Makka anaondokea njia gani

    798- عَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ: أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ ﷺ دَخَلَ مَكَّةَ مِنْ كَدَاءٍ، مِنْ الثَّنِيَّةِ الْعُلْيَا الَّتِي بِالْبَطْحَاءِ، وَخَرَجَ مِنْ الثَّنِيَّةِ السُّفْلَى. [رواه البخاري: 1576].

    1. Imepokewa kutoka kwa Ibn Umar رضي الله عنهما akisema: “Mtume ﷺ aliingia makka alipotoka Madina kwa njia ya Kidaa ambayo ipo katika Jabal linaloitwa Thaniyyatul ‘Ulya lililo kuwepo bonde la Batw’ha na alipotoka alitoka katika bonde la Thaniyat Sufla.” [Bukhari: 1576]

    UFAFANUZI

    Thaniya ni kijichuguu cha jabali, jabali moja lipo katika sehemu za juu karibu na milima na majabali ya Makka inaitwa Thaniyatul ‘Ulya ambapo unakutana nalo ukiingia katika eneo la Batw’haa na upande wa pili kulikuwepo na kijilima kinaitwa Thaniyat Sufla (yaani kilima cha chini na kile cha kule kilima cha juu.)

    KUTOKA *UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    *JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO! *
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu! ‎
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com

  • NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME ﷺ*Leo Jumatatu, tarehe 18 SHAABANI, 1446, H., sawa na tarehe 17, Febryari, 2025. *WASIA WA 57مئتا وصية من وصايا الرسول ﷺجمعها ورتبها ثم فسرها إلى السواحليةالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME *ﷺ.Zimekusanywa na Kufasiriwa kwa Kiswahili naSayyid Abdulqadir ShareefMTIMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    الوصية السابعة والخمسون

    • «في الدعاء أيضًا»*
      57: Dua ya Kujikinga Asubuhi na Jioni

    عَنْ أُنْسٍ بْنِ مَالِك رَضِيَ اللهُ عَنْه قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللهِ ﷺ لِفَاطِمَةٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهَا :« مَا يَمْنَعُكِ أَنْ تَسْمعِي مَا أُوصِيكِ بِهِ! أَنْ تَقُوْلِي إِذَا أَصْبَحْتِ وَإِذَا أَمْسَيْتِ : يا حَيُّ يا قَيُّومٌ بِرَحْمَتِكَ أَسْتَغِيثُ ، أَصْلِحْ لِي شَأْنِي كُلِّه ، وَلَا تَكِلْنِي إِلَى نَفْسِي طَرْفَةَ عَيْنٍ ».[ رَوَاهُ النَّسَائِيُّ وَالْبَزَّارُ بِإِسْنادِ صَحِيحٍ ٍ]

    Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik رضي الله عنه akisema: “Amesema Mtume ﷺ kumwambia Fatma, binti yake: “Pasiwepo na kitu chochote ambacho kitakuzuia usisikie wasia ninaokupa. Nao ni kwamba unapoamka asubuhi au jioni kwenda kulala sema; Ewe Mola Uliye hai, mwenye kusimama bila ya kutegemea chochote. Naomba Rehema Yako Uniteremshie na nitengenezee jambo langu lote hili na wala Usiniwakilishe juu ya nafsi yangu hata kwa mpepeso mmoja.” Ameipokea Nasai na Bazaar kwa Isnadi nzuri.

    KUTOKA NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIYA YA MTUME ﷺ
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu
    kcwajawema@gmail.com

  • WASIYA NA MUONGOZO WA MTUME ﷺ KUHUSU NUSU YA PILI YA MWEZI WA SHAABANI

    219- باب النَّهْي عن تقدّم رمضانَ بصوم بعد نصف شعبان إلاَّ لمن وصله بما قبله ، أو وافق عادةً له بأن كان عادته صوم الاثنين والخميس فوافقه

    1. Mlango wa kukatazwa kufunga baada ya nusu ya pili ya Mwezi wa Shaabani ila kwa yule ambaye anaendeleza kufunga alikokuanza kabla ya hapo, au anaendeleza kawaida yake 1232- عن أَبي هُريرة رضيَ اللَّه عَنْهُ ، عن النبيِّ ﷺ قال: « لا يتَقَدَّمَنَّ أَحَدُكمْ رَمَضَانَ بِصَومِ يومٍ أَوْ يومَيْنِ ، إِلاَّ أَن يَكونَ رَجُلٌ كَانَ يصُومُ صَوْمَهُ ، فَلْيَصُمْ ذلكَ اليوْمَ» متفقٌ عليه
      1. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ: “Asitangulie, mmoja wenu, kufunga Mwezi wa Ramadhani kwa siku moja au mbili, ila ikiwa siku hiyo inawiana na siku ya kawaida yake ya kufunga. Kama ni hivyo, basi anaweza kufunga.” Muttafaq ‘alayhi.
        1233- وعن ابنِ عباسٍ ، رضيَ اللَّه عنهما ، قال : قالَ رسولُ اللَّهِ ﷺ : « لا تَصُومُوا قَبْلَ رَمَضَانَ ، صُومُوا لِرُؤْيتِهِ ، وَأَفْطِرُوا لِرُؤْيَتِهِ ، فَإِنْ حالَتْ دُونَهُ غَيَايةٌ فأَكْمِلوا ثَلاثِينَ يوماً » رواه الترمذي وقال : حديث حسنٌ صحيحٌ. « الغَيايَة » بالغين المعجمة وبالياءِ المثناةِ من تحت المكررةِ ، وهِي : السَّحَابةُ .
      2. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Abbas رضي الله عنهما akisema: Amesema Mtume ﷺ: “Msifunge kabla ya Mwezi wa Ramadhani; fungeni kwa kuona andamo la Mwezi na fungueni kwa kuona andamo la Mwezi. Mkizuwiwa na mawingu kuona andamo la Mwezi, kamilisheni siku thelathini.” Ameipokea Tirmidhi na kusema: Hadithun Hasanun Swahih
        1234- وعنْ أَبي هُريْرَةَ رضِيَ اللَّه عَنْهُ قال : قالَ رسولُ اللَّهِ ﷺ : « إِذا بَقِيَ نِصْفٌ مِنْ شَعْبانَ فَلا تَصُومُوا » رواه الترمذي وقال : حديثٌ حَسَنٌ صحيحٌ .
      3. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ : “Inaposalia nusu ya Mwezi wa Shaabani msifunge!” Ameipokea Tirmidhi na kusema: Hadithun Hasanun Swahih
        1235- وَعَنْ أَبي اليَقظَان عمارِ بنِ يَاسِرٍ رضيَ اللَّه عنْهما ، قال : « مَنْ صَامَ اليَومَ الَّذِي يُشكُّ فِيهِ فَقَدْ عَصَى أَبا القَاسِمِ ﷺ » رواه أبو داود ، والترمذي وقال : حديثٌ حسن صحيحٌ
      4. Imepokewa kutoka kwa Abulyaqdhaan, ‘Ammar bin Yasir رضي الله عنهما akisema: “Anayefunga (Ramadhani) siku inayotiliwa shaka atakuwa amemuasi Abal-Qasim ﷺ.” Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi aliyesema: Hadithun Hasanun Swahih
        UFAFANUZI
        Hadithi hizi zinatufunza mambo mawili muhimu yenye kuhusiana na Funga ya Ramadhani.
        KWANZA ; inatufunza uharamu wa kutangulia kufunga Ramadhani kwa siku moja au mbili, baada ya kuingia nusu ya pili ya mwezi wa Shaabani, isipo kuwa kwa mtu ambaye siku mbili hizo zinawiana na kawaida yake ya kufunga katika siku hizo, kama Jumatatu na Alhamisi. Venginevyo ni makuruhusu sana. Na iwapo siku hiyo inaangukia tarehe 30 Shaabani, na ikashindikana kuonekana mwezi mwandamo tarehe 29, kuamkia 30 Shaabani, basi ni haramu kufunga siku inayo fuata tarehe 29, yaani tarehe 30 Shaabani, ambayo inajulikana katika Sharia kuwa ni يوم الشك Siku ya Shaka. Hivyo, ni haramu kufunga Siku ya Shaka, pasi na kuonekana mwezi mwandamo tarehe 29 Shaabani, katika nchi ya mhusika. Mtume ﷺ amesema wazi wazi kuwa: “Msifunge kabla ya Mwezi wa Ramadhani; fungeni kwa kuona mwezi mwandamo wa mwezi na fungueni kwa kuona mwandamo wa Mwezi. Mkizuwiwa na mawingu kuona mandamo wa Mwezi, kamilisheni siku thelatini.”, na Sayyidina Ammar bin Yasir رضي الله عنه ameweka wazi kuwa kufunga Siku ya Shaka ni kumuasi Mtume ﷺ . Na kumuasi Mtume ﷺ ni haramu. Hivyo, kufunga siku ya Shaka ni haramu.
        PILI; zinatufunza kuwa kuingia na kutoka kwa Mwezi wa Ramadhani, ni kwa kuona mwezi-mwandamo tu, na SI venginevyo. Na kwamba lau kama itashindikana kuona mwezi mwandamo, kutokana na kutanda mawingi – na mawingu kamwe hayawezi kutanda dunia nzima- na hivyo kufunikwa na mawingu, basi hakuna kufunga siku inayo fuata; maana siku hiyo ndiyo يوم الشك. Na Yawmush-Shakk inaweza kuwa ni siku inayo fuatia tarehe 29 Shaabani, au siku inayo fuatia tarehe 29 Ramadhani; yaani tarehe 30 Shaabani na tarehe 30 Ramadhani ni Siku za Shakka; hivyo haijuzu kufunga tarehe 30 Shaabani, wala kufungua tarehe 30 Ramadhani; pasi na kuthibitika kuonenaka mwezi-mwandamo. Haramu.
        YALIYOMO NA YATOKANAYO
    2. Haramu kuitangulia funga ya Ramadhani kwa siku moja au mbili, isipo kuwa itapo tokea kuwa mojawapo wa siku hizo imewiana na siku yako za kawaida ya kufunga, na hivyo itakuwa kufunga Sunna siyo kufunga Ramadhani.
    3. Wanazuoni wanasema kuwa sababu ya kukatazwa huko ni kufanya swaumu hiyo kuwa ni mazoezi, badala ya kufunga kwa ajili ya Allah.
    4. Haramu kufunga siku ya shaka, nayo ni tarehe 30 Shaabani, pasi na ushahidi thabiti wa kuonekana mwezi mwandamo tarehe 29.
    5. Haramu kutokufunga siku ya shaka ya Ramadhani, nayo ni tarehe 30 Ramadhani, pasi na ushahidi thabiti wa kuonekana mwezi mwandamo tarhe 29 Ramadhani.
    6. Pasipo onekana mwezi mwandamo, tarehe 29 Shaabani basi ni wajibu kukamilisha Shaabani siku 30.
    7. Pasipo onekana mwezi mwandamo, tarhe 29 Ramadhani, basi ni wajibu kukamilisha Ramadhani siku 30.
    8. Mwenye kufunga au kufungua siku ya shaka amemuasi Mtume ﷺ .

    والله أعلم

    وبالله التوفيق

    HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ ‎
    Limejibiwa na Sayyid Abdulqadir Shareef
    *Mtumishi wa Sunna za Mtume ﷺ *

    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية

    JIUNGE NA KUMBI ZA DARSA ZA SAYYID ABDULQADIR SHAREEF, KWA KUTUMA MAMBO YAKO MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887, KUPITIA WHATSAP TAJA MAJINA YAKO HALISI MATATU NA MAHALI ULIPO! SHARIA ZA MITANDAO TANZANIA
    UKIWA NA SUALA LOLOTE, LINALOKUHUSU WEWE MWENYEWE, NA SI KUMHUSU MTU MWENGINE, USIMTUMIE MWENYE KUTOA DARSA, BALI MTUMIE ADMIN WA UKUMBI WAKO, AKUPATIE JIBU, KAMA LIPO JIBU LAKE, KUTOKANA NA MAJIBU ZAIDI YA 3000, AU ALIWEKE SUALA LAKO KUMBINI, LISUBIRI KUJIBIWA! USIMTUMIEA MTOA DARSA

    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com

  • KCWW 71\2 MLANGO WA UNYENYEKEVU NA UUNGWANA‎

    Hadithi ya Marudio Jumapili, tarehe 17, Shaabani, 1446, sawa na 16 ‎Februari, 2025.‎‏‎ ‎

    SEHEMU YA PILI.‎

    KUHUSU FADHILA ZA UNYENYEKEVU NA UUNGWANA

    ‎71- Mlango wa unyenyekevu na uungwana kwa waumini.

    Amesema Mwenyezi Mungu ‎سبحانه وتعالي‎ :- ‎

    ‎1.‎ Na wapokee kwa upole wale wanao kufuata miongoni mwa waumini ‎‎(Ash-Shu‘araa’: 215)‎

    ‎2.‎ Enyi mlio amini! Atakaye iacha Dini yake miongoni mwenu, basi ‎Mwenyezi Mungu Ataleta watu Anao wapenda, nao wanampenda, ‎wanyenyekevu kwa Waumini na wenye nguvu juu ya makafiri (Al-‎Ma’ida:54)‎

    ‎3.‎ Enyi watu! Hakika Sisi Tumekuumbeni kutokana na mwanamume na ‎mwanamke, na Tumekujaalieni muwe mataifa na makabila mbali ‎mbali ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi, miongoni mwenu, kwa ‎Mwenyezi Mungu, ni yule aliye mchamungu zaidi kati yenu (Al-‎Hujuraat:13)‎

    ‎4.‎ Basi msijisifu kuwa ni safi nafsi zenu; Yeye Anamjua sana mwenye ‎kujikinga na maovu (An-Najm:32)‎

    ‎5.‎ Na hao watu wa mnyanyukoni watawaita watu wanao wajua kwa ‎alama zao; Watasema: Ujima (umoja) wenu haujakusaidieni kitu, ‎na wala kiburi chenu. Je, hawa sio wale mlio kuwa mkiwaapia kuwa ‎Mwenyezi Mungu Hatawafikishia rehema? Ingieni Peponi, msiwe na ‎khofu, wala msihuzunike (Al-A‘raaf:48-49)‎

    ‎611. Imepokewa kutoka kwa al-Aswad bin Yaziid akisema: Aliulizwa ‎Bi. ‘Aisha ‎‏ رضي الله عنها‎ kitu gani alikuwa anakifanya nyumbani Mtume ‎‏ ﷺ‎? ‎Akasema: “Alikuwa anawahudumia wake zake, na Swala inaponadiwa, basi ‎hutoka kwenda kuswali.” Ameipokea Bukhari. ‎

    ‎612. Imepokewa kutoka kwa Abu Rifa’a Tamiim bin Usayd ‎رضي الله ‏عنه‎ akisema: nilifika kwa Mtume ‎‏ ﷺ‎ nikamkuta anahutubia watu, basi ‎nikasema: “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Mgeni amekuja anauliza ‎kuhusu dini yake. Hajui kitu, kuhusu dini yake!” Akakatiza Mtume ‎ﷺ ‏‎ ‎hutuba yake, na kunijia nilipo. Akaekewa kiti, akakaa. Akaanza kunielimisha ‎alichoelimishwa na Mwenyezi Mungu. Alipomaliza akarudia kuhutubia ‎mpaka akamaliza.” Ameipokea Muslim. ‎

    ‎613. Imepokewa kutoka kwa Anas ‎رضي الله عنه‎ akisema: Alikuwa ‎Mtume ‎‏ ﷺ‎: anapomaliza kula chakula, huramba vidole vyake vitatu [gumba, ‎shahada na kidole cha kati]. Na alisema: ‎

    ‎“Ikidondoka tonge ya mmoja wenu, basi na aiokote, kisha aisafishe na aile; ‎kamwe asiiache kwa Shetani.” na ameamrisha kurambwa bakuli [sahani] na ‎kusema: “ Hamuwezi kujua, baraka ya chakula chenu iko wapi!” Ameipokea ‎Muslim.‎

    ‎614. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra ‎رضي الله عنه‎ akisema: ‎Amesema Mtume ‎‏ ﷺ‎: ‎

    ‎“Kila Mtume aliyepelekwa na Mwenyezi Mungu alichunga mbuzi.” ‎

    Maswahaba wakamuuliza: “Hata wewe?” Akasema:“Ndiyo, hata mimi. ‎Nilikuwa nikiwachunga kwa ujira kutoka kwa wamiliki wake wa Makka.” ‎Ameipokea Bukhari. [Maridio ya Hadithi Nam.605.] ‎

    ‎615. Imepokewa kutoka kwa Abu Huraya ‎رضي الله عنه‎ akisema: Amesema ‎Mtume ‎‏ ﷺ‎: “Lau kama nitaalikwa kwenda kula mguu au mkono wa mbuzi ‎nitaitika. Na lau kama nitazawadiwa mkono au mguu (au hata kwato) wa ‎mbuzi nitaupokea.” Ameipokea Bukhari. ‎

    ‎616. Imepokewa kutoka kwa Anas ‎رضي الله عنه‎ akisema: Alikuwa ‎Mtume ‎‏ ﷺ‎ na ngamia jike, anaitwa: al-‘Adh-baa’. Alikuwa ana kasi kubwa ‎sana; hawezekani kwa kukimbia, na karibu siku zote alikuwa anamshinda ‎mwenye kushindana naye. ‎

    Siku moja, hata hivyo, akatokea bedui, akiwa amepanda kinda lake la ‎ngamia. Akashindana naye, akashindwa. Basi waislamu wakasikitishwa sana ‎na tukio hilo. Mtumeﷺ‎ akahisi kwamba wamesikitishwa kuona al-‘Adh-baa’ ‎ameshindwa. Basi akawapoza kwa kuwaambia:‎

    ‎“Msisikitishwe! Hivyo ndivyo Anavyofanya Mwenyezi Mungu; hakuna kitu ‎kitachopaa juu sana, duniani, ila kuna siku Mwenyezi Mungu Atakiteremsha ‎chini tu.” Ameipokea Bukhari. ‎

    UFAFANUZI

    Kuramba vidole, baada ya kula, na kabla ya kuosha mkono, ni Sunna. ‎Mtume ‎ﷺ‎ alikuwa akiramba vidole vyake vitatu, ambavyo ndivyo ‎alivyokuwa akilia chakula. Na hii inaonesha wazi wazi kuwa Mtume ‎ﷺ‎ ‎alikuwa akila vyakula vinavyoweza kuchukuliwa kwa vidole vitatu, kama ‎tende, mkate wa kuchovya kwenye “mchuzi” au kwenye supu, au nyama ya ‎kuchoma, na hivyo ni vidole hivyo vitatu ndivyo vilivyokuuwa vinaroa ‎chakula tepetepe, kama mchuzi. ‎

    Hivyo basi, chakula chochote kile ambacho hakiwezi kuchotwa kwa vidole ‎vitatu, (kama wali na mchuzi, au ugali na mchuzi) basi kinaweza kuchotwa ‎kwa vidole zaidi ya vitatu, kama vidole vine, au hata vyote vitano; PASI NA ‎KUHUSISHA KIGANJA CHA MKONO. Haya ndiyo maadili ya kula chakula ‎kwa mkono. Mtume ‎ﷺ‎ , siku zote, alikuwa akichota chakula kwa vidole ‎vyake, tu, pasi na kuhusisha kiganja chake; tofauti na watu wengi, wenye ‎kupiga matonge makubwa kabisa, kwa kiganja chote cha mkono, ambalo ‎hawezi kulitia kinywaniu mpaka, kwanzaa, alikamue-kame na kulibinya-‎binya, ili liwe dogo la kuweza kuingizwa kinywani! Huo ni uroho na SI ‎sunna ya Mtume ‎ﷺ‎ . ‎

    Kwa maana hiyo, mitindo yetu ya kuchota tonge kwa mkono wote, vidole ‎vitano na kiganja cha mkono, na kisha KUIVIRINGA VIRINGA TONGE, ‎ILI IWE NDOGO YA KUWEZA KUINGIA MDOMONI ni UROHO na ‎KARAHA na wala SI MAADILI YA KULA. Hakuna haja, wala si busara, ‎kuchota chakula kingi mkononi na kisha kukiminya minya ili kiweze kuingia ‎kinywani! NI UROHO NA SI JAMBO LA KUPENDEZA. Mtume ‎ﷺ‎ ‎hakupata kula kwa kuchanganya kiganja chake cha mkono kuchota chakula. ‎Siku zote kiganja chake cha mkono kilisalia kikavu. ‎

    YALIYOMO NA YATOKANAYO

    ‎1.‎ Ukamilifu wa unyenyekevu wa Mtume ‎ﷺ‎ katika kuwahudumia wake ‎zake nyumbani.‎
    ‎2.‎ Sunna kwa Baba mzazi kusaidia kazi za nyumbani, kadiri ya uwezo ‎wake, na siyo kujigeuza mfalme Sulemani.‎

    ‎3.‎ Hima ya Mtume ‎ﷺ‎ kudumisha Swala katika wakati wake, na ‎kutokubali kushughulishwa na kitu chochote kengine, kufika hadi ‎kuchelewesha Swala katika wakati wake.‎

    ‎4.‎ Unyenyekevu wa Mtume ‎ﷺ‎ katika kuhudumia mambo ya Waislamu ‎wenye kuhitajia zaidi, msaada wake; kama alivyosita kuhutubia ili ‎kumfunza mpita njia aliyetaka aelimishwe kuhusu Dini yake, baadae ‎kurudi kuendelea kutoa hotuba yake. ‎

    ‎5.‎ Umuhimu wa kumjibu, kwa haraka iwezekanvyo, mwenye kuuliza ‎swali la Dini.‎

    ‎6.‎ Wanazuoni wamesema kuwa ni Wajibu kumshughulikia mtu aliyekuja ‎kuuliza kuhusu Imani na Dini yake, haraka iwezekanavyo na SI ‎KUAHIRISHA hadi avunjike moyo. Kama alivyofanya Mtume ‎ﷺ‎ na ‎mgeni huyu.‎

    ‎7.‎ Kujuzu kukatisha hotuba, hata kama hotuba ya Ijumaa, ikitokea ‎udhuru na dharura, na kisha kurudia kuondelea na hotuba.‎

    ‎8.‎ Kukatisha hotuba kwa kutembea hatua chache, au hata kukaa kitako, ‎kutokan na dharura, hakukatishi mfululilozo wa kisharia, hotuba ‎yenyewe. ‎

    ‎9.‎ Sunna ya kula kwa vidole vitatu: Kidole gumba, kidole cha Shahada ‎na kidole cha kaati.‎

    ‎10.‎ Karaha ya kula kwa mkono mzima, kuanzia vidole vitano hadi kiganja ‎cha mkono. Ni ishara ya uroho.‎

    ‎11.‎ Sunna ya kula kwa tonge ndogo ndogo, na si kwa MATONGE ‎MAKUBWA.‎

    ‎12.‎ Suna ya kuramba vidole, BAADA ya kumaliza kula, na kabla ya ‎kuosha mkono.‎

    ‎13.‎ Chakula kikidondoka na kikawa kinaweza kuokotwa na kusafishwa, ‎basi kiokotwe na kusafishwa na kisha kuliwa.‎

    ‎14.‎ Kisicho safishika kisiokotwe na kuliwa; lakini kinaweza kuokotwa na ‎kupewa wanyama wa kufugwa nyumbani, au hata wanayama wapita ‎njia.‎

    ‎15.‎ Sunna ya kuramba bakuli au sahani, baada ya kumaliza kula. Na ‎kuramba huku ni kwa vidole na SI KWA ULIMI, kama anavyo ramba ‎mbwa au paka.‎

    ‎16.‎ Kujuzu kwa waliokula kwa pamoja kuramba sahani au bakuli, kwa ‎vidole vyao na SI KWA NDIMI ZAO.‎

    ‎17.‎ Kila chakula kina baraka iliyofichwa na Mwenyezi Mungu katika ‎chakula hicho au chombo cha chakula hicho.‎

    ‎18.‎ Hima ya Uwislamu na mafunzo yake katika kuhifadhi na kulinda ‎neema za Mwenyezi Mungu.‎

    ‎19.‎ Uharamu wa kumwaga chakula, kwa kisingizio kuwa ni MAKOMBO.‎

    ‎20.‎ Uharamu wa kujaza chakula kwenye sahani, kupindukia uwezo wa ‎walaji kumaliza chakula kile, kiasi kwamba kinachosalia kinatupwa!‎

    ‎21.‎ Kuchunga n’gombe au mbuzi ni kazi ya Mitume, hivyo usimbeze ‎mchunga wanyama.‎

    ‎22.‎ Uhalali wa kupokea ujira kwa huduma halali uliyotoa.‎

    ‎23.‎ Wajibu wa kuitikia mwaliko wa chakula, hata kama ni supu ya miguu ‎ya mbuzi, isipokuwa kama una udhuru.‎

    ‎24.‎ Sunna ya kumualika nduguyo kwenye chakula na Wajibu wa kukubali ‎mwaliko huo; kwani jambo kama hilo ndilo linaloimarisha duguu na ‎mapenzi kati ya watu wawili.‎

    ‎25.‎ Kujuzu kufanya mashindano ya mbio na mfano wake: kama mbio za ‎riyadha, pasi na kucheza kamari. Kwani kamari ni HARAMU.\‎

    ‎26.‎ Kujuzu kumtunukia mshindi zawadi ya ushindi wake, ili kushajiisha ‎mashindano kama hayo ya halali, BILA YA ZAWADI HIYO ‎KUTOKANA NA KAMARI.‎

    ‎27.‎ Kila mshindi ana siku atashindwa; na kila kipandacho juu kuna siku ‎kitateremshwa chini. Hiyo ni KAWAIDA ya Mwenyezi Mungu kwa ‎viumbe vyake.‎

    ‎28.‎ Ukishindwa ukubali kushindwa, kwani hakuna kiumbe ambaye ‎atashinda siku zote. Kukataa kushindwa, unaposhindwa, ni KIRUBI, ‎hivyo ni HARAMU.‎

    والله أعلم
    ‏ ‏
    وبالله التوفيق‎ ‎

    السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم.‏

    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef

    Kutoka Kitabu cha: Kitalu cha Waja Wema: Maneno ya Muokozi ‎wa ‎Umma, ‎ambacho ni tafsiri kamili ya ‎رياض الصالحين من كلام سيد المرسلين للإ ‏مام ‏النووي ‏‎ ‎kilicho tungwa na Imam An-Nawawi na kufasiriwa kwa ‎Kiswahili na ‎Sayyid ‎Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim ‎آل الشيخ ابى بكر بن ‏سالم‎.‎

    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako au kwenye ‎WhatsApp na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.‎

    kcwajawema@gmail.com

  • NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME ﷺ*Leo Jumatatu, tarehe SHAABANI, 1446, H., sawa na tarehe 15, Febryari, 2025. *WASIA WA 56مئتا وصية من وصايا الرسول ﷺجمعها ورتبها ثم فسرها إلى السواحليةالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIA ZA MTUME *ﷺ.Zimekusanywa na Kufasiriwa kwa Kiswahili naSayyid Abdulqadir ShareefMTIMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    الوصية السادسة والخمسون

    • «تعويذة من العقرب»*
      56: Kinga ya kuumwa na Nge

    عَنْ أُبِيَ هُرَيْرَة رَضِيَ اللهُ عَنْه قَال : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبِيِّ ﷺ فَقَال : يا رَسُولَ اللهِ مَا لَقِيتُ مِنْ عَقْرَبٍ لَدَغْتْنِي الْبَارِحَةَ ، قَالَ :« أَمَّا لَوْ قُلْتَ حِينَ أَمْسَيْتَ : أَعُوذُ بِكَلِمَاتٍ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرٍّ مَا خَلْقَ ، لَمْ تَضُرْكَ »[ رَوَاهُ مَالِكٌ وَمُسْلِمٌ وَالتِّرْمِذِيُّ وَحُسْنَهُ ] وَلَفَظَهُ :« مِنْ قَالٍ حِينَ يُمْسِي ثَلاثَ مَرَّاتٍ : أَعُوذُ بِكَلِمَاتٍ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرٍّ مَا خَلْقَ ، لَمْ يَضُرُّهُ حَمَة تِلْكَ اللَّيْلَة ». قَالَ سُهَيْلٌ : فَكَانَ أهْلُنَا تَعَلَّمُوهَا فَكَانُوا يَقُولُونَهَا كُلُّ لَيْلَةٍ فَلُدِغْتْ جَارِيَة مِنْهُمْ فَلَمْ تَجِدْ لَهَا وَجَعًا .[ رَوَاهُ اِبْنُ حُبَّانٍ فِي صَحِيحِهِ ]

    Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضي الله عنه akisema: “Mtu mmoja alimuendea Mtume ﷺ akasema: “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nimepata maumivu makubwa sana jana usiku kutokana na kung’atwa na Nge.” Mtume ﷺ akasema: “Lau kama ungelisema kabla ya kwenda kulala; Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyo kamilika kutokana na kila shari Aliyoiumba, Nge huyo asingeweza kukudhuru.” Ameipokea Malik, Muslim na Tirmidhi. Riwaya nyingine inasema: “Mwenye kusema mara tatu maneno hayo pale anapokwenda kulala, hatadhuriwa na jambo lolote usiku ule.” Amesema Suhaib: “Pale tulipo wafundisha watoto wetu maneno hayo kusema kila usiku, usiku mmoja mjakazi wetu aliumwa na Nge lakini hakupata maumivu yoyote.” Ameipokea Ibn Hibban katika Sahihi yake.

    KUTOKA NYASIA 200 MIONGONI MWA NYASIYA YA MTUME ﷺ
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu
    kcwajawema@gmail.com

  • TAFSIRI YA UFUPISHO WA KITABU CHA SWAHIHIL-BUKHARIمختصر صحيح البخاري للزبيديرتبه ثم فسره إلى السواحلية ووضع بعض تعليقاتالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*TAFSIRI YA UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY.*Kimetayarishwa kisha Kufasiriwa kwa Kiswahili *Sayyid Abdulqadir ShareefMTUMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    Leo Siku ya Ijumaa, tarehe 15, Shaaban 1446, H., sawa na tarehe 14 Februari, 2025.

    20- بَاب: قَوْلِ اللَّهِ تعالى: ]الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَعْلُومَاتٌ[ إلى قوله: ]فِي الْحَجِّ[ [البقرة: 197]

    1. Mlango: Maana ya maneno ya Mwenyezi Mungu: Hijja ni miezi maalum. Aya kamili [Al-Baqara:197]

    789- عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهَا، حديثها فِي الحَجِّ قَدْ تَقَدَّمَ،( ) قَالَتْ فِي هذِهِ الرَّوايَةِ: خَرَجْنَا مَعَ رَسُولِ اللَّهِ ﷺ فِي أَشْهُرِ الْحَجِّ، وَلَيَالِي الْحَجِّ، وَحُرُمِ الْحَجِّ،( ) فَنَزَلْنَا بِسَرِفَ، قَالَتْ: فَخَرَجَ إِلَى أَصْحَابِهِ فَقَالَ: «مَنْ لَمْ يَكُنْ مِنْكُمْ مَعَهُ هَدْيٌ، فَأَحَبَّ أَنْ يَجْعَلَهَا عُمْرَةً فَلْيَفْعَلْ، وَمَنْ كَانَ مَعَهُ الْهَدْيُ فَلَا» قَالَتْ: فَالْآخِذُ بِهَا وَالتَّارِكُ لَهَا مِنْ أَصْحَابِهِ، قَالَتْ: فَأَمَّا رَسُولُ اللَّهِ ﷺ وَرِجَالٌ مِنْ أَصْحَابِهِ، فَكَانُوا أَهْلَ قُوَّةٍ، وَكَانَ مَعَهُمْ الْهَدْيُ، فَلَمْ يَقْدِرُوا عَلَى الْعُمْرَةِ. وَذَكَرَ بَاقِي الحَدِيثِ. [رواه البخاري: 1560].

    1. Imepokewa kutoka kwa Aisha رضي الله عنها ambayo imekwisha tangulia, hapa anataja mambo ya Hijja katika riwaya hii ya sasa anasema: “Tulitoka na Mtume ﷺ katika miezi ya Hijja, na katika mchana ya siku za Hijja na katika siku zinazokatazwa kufanya mambo mambo yoyote ndani ya mwezi wa Hijja, tukaenda na kusafiri mpaka tukafika eneo la Sarfu, akatoka Mtume ﷺ kwenda kwa maswahaba wake na kuwaambia: “Yeyote katika nyinyi ambaye hakuswaga mnyama wa kuchinja Minaa na akapenda kufanya Umra kisha avue nguo zake afanye, lakini yeyote yule ambaye ameswaga mnyama wake wa Hijja basi akishafanya Umra asivue nguo zake, asalie mpaka amalize kufanya Hijja” Anasema Aisha: “Hivyo wapo watu katika maswahaba wake ambao waliochukua ushauri huo wakavua nguzo za Umra na kusubiri Hijja na wapo ambao hawakufanya hivyo mpaka wakamaliza Hijja” anasema Aisha: “Ama Mtume ﷺ na baadhi ya maswahaba wake walikuwa ni kikundi kikubwa kidogo na walikuwa kila mmoja amemswaga mnyama wake kwa hivyo hawakuweza kuvua nguo baada ya Umra” akayamaliza maneno yake yakaendelea mpaka mwisho wa hadithi.” [Bukhari: 1560]

    KUTOKA *UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    *JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO! *
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu! ‎
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com

  • TAFSIRI YA UFUPISHO WA KITABU CHA SWAHIHIL-BUKHARIمختصر صحيح البخاري للزبيديرتبه ثم فسره إلى السواحلية ووضع بعض تعليقاتالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*TAFSIRI YA UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY.*Kimetayarishwa kisha Kufasiriwa kwa Kiswahili *Sayyid Abdulqadir ShareefMTUMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    Leo Siku ya Alkhamis, tarehe 14, Shaaban 1446, H., sawa na tarehe 13 Februari, 2025.

    19- بَاب: مَنْ أَهَلَّ فِي زَمَنِ النَّبِيِّ ﷺ كَإِهْلَالِ النَّبِيِّ ﷺ

    1. Mlango: walio nuia Hijja katika zama za Mtume ﷺ kama alivyo nuia Mtume ﷺ

    788- عَنْ أَبِي مُوسَى رضي الله عنه قَالَ: بَعَثَنِي النَّبِيُّ ﷺ إِلَى قَوْمٍ بِالْيَمَنِ، فَجِئْتُ وَهُوَ بِالْبَطْحَاءِ، فَقَالَ: «بِمَا أَهْلَلْتَ؟» قُلْتُ: أَهْلَلْتُ كَإِهْلَالِ النَّبِيِّ ﷺ ، قَالَ: «هَلْ مَعَكَ مِنْ هَدْيٍ؟» قُلْتُ: لَا، فَأَمَرَنِي فَطُفْتُ بِالْبَيْتِ وَبِالصَّفَا وَالْمَرْوَةِ، ثُمَّ أَمَرَنِي فَأَحْلَلْتُ، فَأَتَيْتُ امْرَأَةً مِنْ قَوْمِي، فَمَشَطَتْنِي، أَوْ غَسَلَتْ رَأْسِي.فَقَدِمَ عُمَرُ رضي الله عنه فَقَالَ: إِنْ نَأْخُذْ بِكِتَابِ اللَّهِ فَإِنَّهُ يَأْمُرُنَا بِالتَّمَامِ، قَالَ اللَّهُ: ]وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّهِ[ [البقرة: 196]. وَإِنْ نَأْخُذْ بِسُنَّةِ النَّبِيِّ ﷺ فَإِنَّهُ لَمْ يَحِلَّ حَتَّى نَحَرَ الْهَدْيَ. [رواه البخاري: 1559].

    1. Imepokewa kutoka kwa Abu Musa رضي الله عنه akisema: “Mtume ﷺ alinituma kwenda kwa watu wa Yemen, niliporudi nikamkuta yupo katika eneo la Batwhaa, akaniuliza: “Umenuia vipi ibada yako?” akasema: “Nimenuia kama alivyonuia Mtume ﷺ “ Mtume ﷺ akamuuliza: “Je umeswaga mnyama wako wa kuchinja?” nikasema: “Hapana” basi akanambia: “Kama ni hivyo katufu Al Ka’ba, nenda Swafa na Marwa na ukimaliza vua nguo baada ya kunyoa au kupunguza” anasema: Nikaenda kwa mke wangu, nikafanya nae haja baada ya kukoga, akanichana nywele au akanikosha kichwa changu, baadae Umar akatokeza, nikamueleza nilichofanya lakini akanijibu: “Sisi tunafuata kitabu cha Mwenyezi Mungu, ametuamrisha kukamilisha vitu viwili, amesema Mwenyezi Mungu:Na timizeni Hijja na Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. (Al-Baqara: 196) na kwa ajili hiyo tunafuata sunna ya Mtume ﷺ kwani Mtume ﷺ alipokuwa amekuja akiwa ameswaga mnyama wake hakuvua nguo zake baada ya Umra alikaa mpaka akaenda akafanya Hijja na kumaliza.” [Bukhari: 1559]

    KUTOKA *UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    *JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO! *
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu! ‎
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com

  • Hadithi ya Leo, Alhamisi, tarehe 14, Shaabani, 1446, sawa na tarehe 13, JANUARI, 2025

    KUHUSU KUCHINJA MNYAMA WA AQIQA

    SEHEMU YA TATU

    1359 – وَعَنْ سَمُرَةَ بن جندب رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: { “كُلُّ غُلَامٍ مُرْتَهَنٌ بِعَقِيقَتِهِ، تُذْبَحُ عَنْهُ يَوْمَ سَابِعِهِ، وَيُحْلَقُ، وَيُسَمَّى” } رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيّ .

    1. Imepokewa kutoka kwa Samurah رضي الله عنه akisema: “Amesema Mtume : “Kila mtoto atakuwa amewekwa rahani kwa mbuzi wake wa Aqiqa mpaka mbuzi wake huyo achinjwe siku ya saba kisha anyolewe nywele na apewe jina.” Wameipokea Maimamu watano na ameisahihisha Tirmidhi.

    UFFAFANUZI

    Hadithi hii, inayotufungia mlango huu wa Aqiqa, inatuzindua kuhusu umuhimu wa kumchinjia mtoto wa kiume, mnaya wa Aqiqa, kwani yeye ndiye atayekuja kuendeleza kizazi na nasaba ya Baba mtu. Mtume ﷺ amepiga mfano wa kuweka kitu Rahani, ambacho humaanisha kuwa kitu kilichowekwa Rahani lazima kikakombolewe kwa wakati wake, venginevyo kinaweza kuchukuliwa na mwenye mamlaka ya Rahani. Na kwa maana hiyo, mtoto wa kiume hatoweza kutekeleza majukumu yake kwa Baba yake, iwapo atakuwa hajachinjiwa mnyama wa Aqiqa, tena ndani ya wakati wake, nao ni ndani ya siku saba tokea kuzaliwa, na atimiziwe mambo mengine, kama kumnyoa nywele zake na kumpa jina. Imam Ahmad amefafanua kwa kusema kuwa “Mtoto asiyetimiziwa Ibada hiyo, hatokuwa mionngoni mwa wataomuombea Sha’faa Baba yake siku ya Kiyama. Kwa maneno mengine, mtoto asiyechinjiwa mnyama wa Aqiqa, na kutekelezewa utaratibu wake, licha ya Baba mzazi kuwa na uwezo wa hali na mali, bila ya kufanyiwa Ibada hiyo, hatojaaliwa kuwa mwana mwema kwa Baba yake. Na iwapo atatokea kuja kufariki, bila ya kufanyiwa Ibada hiyo, ndani ya wakati wake, basi Baba mtu atakuwa amepoteza fursa ya kunufaika na mtoto wake huyo; hapa Duniani na huko Akhera. Hivyo, ni muhimu sana kwa Wazazi wa mtoto wa kiume, kumchinjia mtoto wao huyo, wanyama wa Aqiqa, ndani ya siku saba, tokea kuzaliwa. Na hiyo ndiyo maana ya maneno ya Mtume ﷺ yasemayoi: “Kila mtoto atakuwa amewekwa rehani kwa mbuzi wake wa Aqiqa mpaka mbuzi wake huyo achinjwe siku ya saba kisha anyolewe nywele na apewe jina.” 
    
    Zaidi, ni kwamba kila mzazi atasailiwa Siku ya Kiyama kuhusu kuwahi kumchinjia mtoto wake mnyama wa Aqiqa. 

    عن بريدة بن الحصيب قال: “إنَّ النَّاس يعرضون يوم القيامة على العقيقة، كما يعرضون على الصلوات الخمس” رواه البيهقى
    Imepokewa kutoka kwa Burayda bin Al-Haswib akisema: “Amesema Mtume ﷺ: “Watu watasailiwa, Siku ya Kiyama, kuhusu Aqiqa, kama watavyo sailiwa kuhusu Swala tano za kila siku.” Ameipokea Al-Bayhaqi.

    YALIYOMO NA YATOKANAYO

    1. Hadithi hii inatilia mkazo mkubwa Asasi ya Aqiqa, jambo ambalo linamaanisha kutopuuzwa na kuachwa kuteelezwa kwa hali yoyote ile.
    2. Aqiqa ni Ibada inayotakikana kutekelezwa haraka, mara baada ya kuzaliwa mtoto, aghalabu baada ya siku ya saa tokea kuzaliwa.
    3. Muhimu kudiriki haraka kumchinjia mtoto au watoto mnyama wa Aqiqa, akiwa bado yuhai; maana akifariki kabla ya kuchinjiwa mnyama wa Aqiqa, basi mzazi husika atakuwa amejinyima kunufaika na mtoto wake huyo, Duniani na Akhera.
    4. Mweenye kuhuyisha Asasi ya Aqiqa atakuwa amehuyisha Sunna ya Mtume ﷺ aliyoamrisha iteikelezwa, kwa kaulni na vitendo.
    5. Jukumu la kujitolea kuchinja mnyama wa Aqiqa, lipo juu ya mabega ya Baba mzazi wa mtoto husika; ila hakuna junaha kwa mama mzazi naye kuitekeleza Ibada hiyo, panapotokea kuwa Baba mhusika han uwezo wa hali au mali.
    6. Mtoto aliyekosa kuchinjiwa mnyama wa Aqiqa na wazee wake, anaruhusiwa kujichinjia mwenyewe ukubwani.

    MWISHO WA KITABU CHA VYAKULA KITABU KIFUATACHYO NI KITABU CHA YAMINI NA NADHIRI

    والله أعلم

    وبالله التوفيق

    HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO‎ ‎
    IMETAYARISHWA na Sayyid Abdulqadir Shareef
    *Mtumishi wa Sunna za Mtume ﷺ *

    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية

    KUTOKA KITABU CHA بلوغ المرام من أدلة الأحكام UFIKIAJI WA MALENGO KUPITIA HADITHI ZA FIQHI YA MILANGO

    JIUNGE NA KUMBI ZA DARSA ZA SAYYID ABDULQADIR SHAREEF, KWA KUTUMA MAOMBI YAKO, MOJA KWA MOJA, KWENDA NAMBA +255786887887, KUPITIA WHATSAP
    LAZIMA UTAJE MAJINA YAKO HALISI MATATU NA MAHALI ULIPO! SHARIA ZA MITANDAO TANZANIA

    UKIWA NA SUALA LOLOTE, LINALOKUHUSU WEWE MWENYEWE, NA SI KUMHUSU MTU MWENGINE, USIMTUMIE MWENYE KUTOA DARSA, BALI MTUMIE ADMIN WA UKUMBI WAKO, AKUPATIE JIBU, KAMA LIPO JIBU LAKE, KUTOKANA NA MAJIBU ZAIDI YA 3000, AU ALIWEKE SUALA LAKO KUMBINI, LISUBIRI KUJIBIWA USIMTUMIEA MTOA DARSA

    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com

  • TAFSIRI YA UFUPISHO WA KITABU CHA SWAHIHIL-BUKHARIمختصر صحيح البخاري للزبيديرتبه ثم فسره إلى السواحلية ووضع بعض تعليقاتالسيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم العلوي الحسينيخادم السنة النبوية*TAFSIRI YA UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY.*Kimetayarishwa kisha Kufasiriwa kwa Kiswahili *Sayyid Abdulqadir ShareefMTUMISHI WA HADITHI ZA MTUME

    Leo Siku ya Jumatano, tarehe 13, Shaaban 1446, H., sawa na tarehe 12 Februari, 2025.

    18- بَاب: التَّلْبِيَةِ إِذَا انْحَدَرَ فِي الْوَادِي

    1. Mlango: Kupiga Talbiya mtu anapoteremka kwenye bonde lolote

    787- عَنِ ابْنُ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ ﷺ: «أَمَّا مُوسَى: كَأَنِّي أَنْظُرُ إِلَيْهِ، إِذْا انْحَدَرَ فِي الْوَادِي يُلَبِّي».( ) [رواه البخاري: 1555].

    1. Imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas رضي الله عنهما akisema: “Amesema Mtume ﷺ : “Ama Musa: Namuona kwa macho yangu hivi sasa anateremka kwenye bonde la Dhul Hulayfa akipiga talbiya.” [Bukhari: 1555]

    KUTOKA *UFUPISHO WA SWAHIHIL-BUKHARI, YA AZ-ZABIIDY
    *HIFADHI NDANI YA SIMU YAKO ILI UWEZE KUMTUMIA MWENZAKO!‎ *
    *JIUNGE NA DARSA HIZI KWA KUTUMA MAJINA YAKO HALISI MATATU, TAJA MAHALI ULIPO NA WEKA NAMBA YA SIMU ULIOSAJILIWA JINA LAKO! *
    TUMA MOJA KWA MOJA KWENDA +255786887887 –Kupitia Whatsap tu! ‎
    من السيد عبد القادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
    خادم السنة النبوية
    Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef*
    *Mrumiahi wa Hadithi za Mtume ﷺ *
    NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.
    kcwajawema@gmail.com